Sunday 20 April 2014

tiba ya kutoelewana ndani ya familia kati ya mke na mume


Ikitokea kutoelewana kumezidi na hakuna sababu ya msingi, dawa nikupata mafuta yenye nguvu yanayoitwa powerful oil ili kuondoa negative energy miongoni mwa wanandoa kujipaka kila jioni mafuta haya yenye baraka za Mungu kwani yametajwa kwenye Injili, Taurati na Qur'an na miti yake imetajwa mara kadhaa kwenye vitabu vitakatifu.

 Pamoja na tiba hii fuata taratibu hizi:

Kwanza kabisa heshima iwepo na misingi ya ndoa izingatiwe na wote mwanamke na mme wasiwe wanazini nje ya ndoa ili upendo wa miongoni mwao uwepo.

Mwanamke awe msafi kwa ujumla na nyumba iwe safi
Majukumu ya huduma kwa mme asiachiwe msichana wa kazi(House girl) mpaka kumkaribisha kula chakula meza ni msichana, kutandika kitanda, kumchagulia nguo ya kuvaa na kuandaa maji ya kuoga ni msichana, sasa hapa msichana atapendwa kwa huduma zake kwa mme wako na hii si sawa na matokea yatakuwa mabaya kindoa.

Mwanamke ahakikishe anasimamia chakula inakuwa tayari mapema na hasa jioni iive mapema kuanzia saa 2 hadi saa 3 ikiwezekana saa tatu chakula iwe mezani na hii itamfanya mwanaume anayependa vijiwe kuja mapema kula na kupumzika na mke wake mapema.

Wapende ndugu kutoka sehemu mbili kwa mume na mke kama kuna shida katika ndugu mwambie ukweli na muombe aache tabia mbaya na siyo kumsema kwani mtu yoyote ukimsema na akaambiwa na watu wengi makosa yake kuwa wewe ndo umewambia jamaa wengine uchukia sana na kuona kuwa hana kosa ila wewe ndo mbaya umempiga fitina, lakini ukimueleza na ushahidi unao huwa anakuheshimu na kubadilika.

Mwanamke hakikisha unakuwa smart na unajali usafi wako binafsi unaoga na kuwa safi ukiwa nyumbani na pia mletee zawadi mke wako hata chips au apple au anachopenda sana kati ya vitu unavyoweza na hata nguo mara moja moja si mbaya.

Fanya kazi kwa bidii hasa mwanaume ili upate uchumi mzuri kwani mwanaume ukikosa uchumi hata mapenzi yapotea haraka na heshima inashuka kwa speek kali sana, jibu la hili kubuni vyanzo vya uchumi na hasa uchumi ukiwa mbaya usitangaze haraka kwa mke wako na kwa jamaa ila parangana kutafuta vyanzo vya uchumi na Mungu atakusaidia.

Hakikisha unakula tikiti maji(water melon) angalau kila jioni, kunywa tangawizi na karanga kiasi ili kuwa na nguvu na hisia nzuri kama siku hiyo unataka kufanya tendo la ndoa, pia hakikisha unamridhisha mke wake mpaka akwambie nimefika kileleni kama unamuacha njiani ni tatizo na hii itapunguza mapenzi kwako na kama kuna mtu alikuwa amemuoa au alikwa anampenda kabla yako na alikuwa anamfikisha kileleni ni hatari ya kumpigia simu baadhi ya siku ili amridhishe! Hii imetokea mara nyingi kwa watu na kesi tumeziamua bila kuisha na mwisho mume anatulia au mke anatoka kwa mume.

hakikisha unatulia wakati wa tendo la ndoa na kufanya kwa pozi ili usimalize haraka kabla ya mwenzako hajafika kileleni na hii ni tiba kubwa ukimridhisha mwenzio kitandani akasema ahsante sana, lakini ukiona mmemaliza na akatoka amekasirika ujue kuwa unaandaa mazingira ya shida na chuki kwenye ndoa yenu. Hii hata mwanamke ajiandae mapema na kuwa tayari kwa kazi muhimu ya lengo kuu la kuwa mke na mme na kuzaa watoto inapitia kitendo hiki kwa hiyo si mchezo.

Hakikisha matatizo yaliyopo unayasema baada ya tendo hili kwani akili zikiwa zimetulia ndo na tendo ufanyika kwa raha na vizuri zaidi na ndo maana wanasema ukiwa na mawazo mengi hata hamu ya tendo la ndoa inakuwa hakuna, hii ni kuandaa mazingira ya uchumi na kujitahidi kuwa na akili zilizotua na subira katika maisha ili ubunifu wa njia za kiuchumi uwe imara kila kukicha uongeze kipato na mapenzi yatakuwa imara kwani mtakula mshibe, msomeshe watoto na msaidie ndugu lakini ikitokea mara chakula hakipo, mara karo imekosa, mara mama mgonjwa yuko hospitali na huna pesa ya kumtibisha basi akili zinakosa nguvu na kujifunga na hata mapenzi hayafanyiki ipasavyo kwani hamu hakuna ni kufikiri matatizo hayo yanayokuwa mezani bila jibu la haraka.

Kama mwanamke hafanyi zinaa na mwanaume hafanyi zinaa watapendana lakini ikitokea mmoja akaanza basi shetani anachochea zinaa zaidi kwa wote na kuwafanya wapende zinaa zaidi kuliko tendo halali lao la ndoa kila mmoja atajifanya amechoka na mwenzie ataona ni bahati ya kukacha kwani anakuwa ameshiba nje ya ndoa.

Tuwasiliane, Tutakuhudumia na Mungu atasaidia!
Email: tibaherbs@gmail.com 

 +255762053174/+255621870342

No comments:

Post a Comment